Posts

Showing posts from April, 2017

HARMORAPA APATA MUALIKO CANADA

Image
Msanii Harmorapa anaetamba NA Kibao chake  cha kiboko ya Mabishoo Hivi juzi alipata mualiko Nchini Canada. Harmorapa NA shabiki wake Harmorapa  hivi majuzi alifanya  Show ya kihistoria ilio kusanya nashabiki Lukuki na kumfanya aandike historia mpya Katika viwanja vya Dar Live Show hiyo aliofanya na Msanii nguli Juma nature ambae walishirikiana  Pamoja katika nyimbo hiyo ambayo  Imeshika nafasi za juu katika vituo Mbali mbali vya radio NA TV. Hivyo NA kumfanya Msanii Huyo kufahamika zaidi Duniani kote Harmorapa  NA Amber lulu Msanii Harmorapa amekua gumzo Sana katika mitandao ya kijamii  Baada pia kuhusishwa kimapenzi NA Msanii  Wa mitindo katika video kwa jina la Amber lulu Vyanzo kadhaa vya habari vilimuhoji Msanii huyo wa kike  Na kumuuliza kuhusu sakata hill la Kutoka kimahusiano na Kiboko ya Mabishoo. Amber Lulu alidhibitisha hili. Ila siku zilivyozidi kuyoyoma Msanii  Harmorapa alionekana kujihusisha kimahusiano

HALI TETE MKUTANO WA ROMA NA WAANDISHI

Image
Dar es Salaam. Hali ya sintofahamu imeanza kujitokeza tokea leo asubuhi hadi saa 5: 48 baada ya mkutano aliotakiwa kuufanya Roma Mkatoliki na waandishi wa habari kushindwa kufanyika kwa wakati.  Mapema leo kaka yake Roma, Omary Musa amesema mkutano huo ungefanyika saa tano.  Hata hivyo Musa hakuweka wazi eneo la kufanyia mkutano huo kwa kile alichodai bado hawajapata eneo. "Eneo tulilopata awali mwenyewe anaonekana kuwa na hofu, tunatafuta eneo lingine tutawajulisha kabla ya saa tano ila tunalenga maeneo ya Kinondoni, "amesema  Ilipofika saa tano mwandishi alimtafuta kujua eneo Musa akajibu bado hawajapata na huenda mkutano huo ungesogezwa hadi saa nane. "Bado tunatafuta kuna watu wamepewa jukumu hilo, hatuwezi kufanyia popote lazima liwe eneo salama, hatujui waliomteka walikuwa na nia gani".. .

SHOW YA NEYO DAIMOND UTATANI KUSWEKWA RUMANDE

Image
Msanii NASIBU ABDUL (Diamond) Anakaribia kua katika wakati mgumu  Baada ya kupata misuko suko ya kuandaa Show huko marekani bila mafanikio Yaliotarajiwa. Diamond plutnumz Msanii huyo alikua katika mipango ya kufanya show  na msanii mkali wa RNB Marekai NEYO.. Show hizo ambazo zilikua chini ya kazi za Neyo ambapo alipanga kuzunguka mabara  Diamond alipata fursa ya kualikwa na NEYO Kupitia kazi moja ambayo walifanya  Kurekodi mziki wa (merry you) .. Mashabiki wa Mziki ambao Walitenga muda wao kuhudhuria  Show hizo iliokua imeahirishwa  Hadi tarehe 8 April 2017. Ila sintofahamu zilizidi kutokea  Baada ya show hiyo kupelekwa mbele tena Hadi Mwisho wa mwaka 2017. .. .. Mashabiki wengi wamekua na Sintofahamu kwa Kuvurigiwa ratiba zao ambazo walizipanga Huku wengi wakiwa wameshanunua tiketi. .. DAIMOND KIZIMBANI Hivyo uongozi wa Neyo umepata wakati mgumu zaidi baada ya Mashabiki wengi kutaka warudishiwe pesa zao... NA wengine ku

ROMA NA WENZAKE WAPATIKANA

Image
Zilizotufikia: Roma na wenzake wapatikana wakiwa salama ________________________________________ Taarifa zilizotufikia zimedai kuwa Roma na watu wengine waliokuwa wameshikiliwa tangu Jumatano hii wamepatikana wakiwa salama. Bado hakuna maelezo ya kutosha kuhusiana na wapi walipokuwa na nani waliokuwa wamewashikilia. Kwa sasa wanaidaiwa kuwa katika kituo cha polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam kwa taratibu za kipolisi kwakuwa jalada la kupotea kwao lilifunguliwa hapo. Kupatikana kwao kumefuatia wito mkubwa uliokuwa ukipaishwa na wasanii wenzake na mashabiki kuhusu kuachiliwa huru. Awali, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishina Simon Sirro alisema bado walikuwa wakiendelea na upelelezi wa tukio la kupotea (kutekwa) kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake. Akiongea na waandishi wa habari mchana huu Polisi Central jijini Dar es salaam, Kamanda Sirro alisema tukio la utekwaji wa Roma na wenzake ni aina ya matukio ambayo hutokea mara kwa mara. “Matukio