HARMORAPA AICHANGIA ZANZIBAR

Msanii wa Muziki wa Hip Hop Tanzania
Anaejulikana kwa jina HARMORAPA
Kwa hali  ya Matumaini Ameonekana katika kitabu cha Uchangiaji kwa watu wenye mahitaji maalumu Zanzibar...
Harmorapa



Akitoa Ahadi hiyo ya kuchangia kiasi cha pesa cha Dolla 100 Msanii Harmorapa aneonyesha mchango wake na kuguswa na Kampeni hiyo na kumfanya Asimamishe show na kuongea na wananchi waliohudhuria





"Kutokana na matatizo yanayoikumba jamii yetu Mimi Harmorapa kupitia SGS Sabuka Music naahidi kuchangia kiasi cha Dollars 100 kiasi kidogo cha kuwachangia wenye mahitaji."
Alisema HARMORAPA
Harmorapa akiteta na mwandishi


Kampeni hii
imezinduliwa na Mheshimiwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania MH SAMIA SULUHU HASANI na kuhudhuriwa pia na viongozi wengi wa Zanzibar
Harmorapa ambae alikua ni mmoja kati ya wasanii wachache waliolikwa kutumbuizwa katika Tamasha hilo  lililolenga Kuhamasisha uchangiaji wa  Mahitaji ya watu wenye uhitaji lililojulikana kama MIMI NA WEWE.

Makamu Wa Raisi  Tanzania MH.SAMIA SULUHU


Tamasha..
Ambalo lilihudhuriwa na watu wengi ikiwemo wasanii na viongozi.
Ukiachilia Msanii Harmorapa pia walikuepo wasanii wengine kama Benpol Dula makabila , Nandy na wasanii wengi wa Zanzibar.
..
..
Harmorapa ni moja kati ya wasanii waliokua Gumzo katika viwanja vya Kisonge ZANZIBAR  katika Tamasha hill LA MIMI NA WEWE....
..Mashabiki walionyesha kuwa na hamu nae kabla ya kupanda jukwaaani.
kelele za Mashabiki zilisikika zikitaja jina lake Mara tu alipopanda jukwaani.
Harmorapa na Ronei wakitumbuiza Tamasha LA MIMI NA WEWE



Muda huohuo
Akiongea kwa Masikitiko makubwa Mh Makamu wa Raisi Zanzibar ameelezea changamoto zilizoikumba jamii ya watu wa Zanzibar katika kipindi hichi cha Mvua za masika na kuahidi kuchangia jamii hizo kwa kutoa vifaa kadhaa vya ujenzi kusaidia kaya zilizopoteza Nyumba na uharibifu mwingi wa Mali kutokana na halo ya mvua..ikiwa no Moja ya dhamira ya Tamasha hilo..

Comments

Popular posts from this blog

MAHABA ZONE

ORODHA YA WANAUME WA WEMA YAFUNIKA KIMATAIFA

JIKE DUME HILI HAPA